Kampuni ya TanzaniteOne kujenga madarasa saba ya shule ya msingi Songambele ya Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. 

Mkurugenzi wa kampuni ya TanzaniteOne Faisal Juma Shabhai ameahidi kujenga madarasa saba ya shule ya msingi Songambele ya mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, ambayo yameweka ufa. 

Tangu mwaka 2013 madarasa hayo yaliweka ufa kutokana na kupitiwa na
mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha kwenye eneo hilo. 

Kutokana na hali hiyo uongozi wa shule hiyo uliamua kuyafunga madarasa hayo na ofisi ya walimu, wakihofia kupaata madhara kutokana na hitilafu hiyo iliyotokana na tatizo hilo. 

Akizungumza na wananchi wa eneo hilo, Shabhai alisema yeye binafsi atajenga madarasa matatu na wakurugenzi wenzake wa kampuni hiyo Hussein Gonga na Riziwani nao watajenga mengine manne yaliyobakia.
Mkurugenzi wa kampuni ya TanzaniteOne Faisal Shabhai akizungumza kwenye viwanja vya shule ya msingi Songambele Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, alipoahidi wananchi kuwajengea
vyumba saba vya madarasa. 
Mkazi wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara,Japhary Matimbwa akiushukuru uongozi wa kampuni ya TanzaniteOne baada ya kuahidi kujenga madarasa saba ya shule ya msingi Songambele.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara,Jackson Sipitieck akiushukuru uongozi wa kampuni ya TanzaniteOne baada ya kuahidi kujenga madarasa saba ya shule ya msingi Songambele. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...