NA VICTOR MASANGU, KIBAHA.
KATIKA
kuunga juhudi za serikali ya awamu ya tano kupambana na wimbi la
umasikini taasisi ya Namelok ya Wilayani Kibaha inatarajia kujenga kituo
maalumu cha wasichana na wanawake wajasiriamali ambacho kitakuwa
kinajihusisha na masuala ya utoaji wa mafunzo mbali mbali kwa lengo la
kuweza kuwapa fursa ya kuachana na kuwa tegemezi na kujiajiri wao
wenyewe.
Akizungumza
katika sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa kituo hicho zilizofanyika
katika Kata ya Mwendapole iliyopo katika halmashauri ya mji wa Kibaha
Mkurugenzi mtendaji wa taasisi hiyo Janet Mwasuka amesema kukamilika
kwa ujenzi huo kutaweza kuwa ni mkombozi mkubwa wa kuwainua wanawake
hao kiuchumuni kupitia mafunzo ya stadi za kazi pamoja na fursa
zilizopo kutokana na elimu watakayoipata.
Janet
alibainisha kuwa anatambau kuwa wanawake wegine katika Wilaya ya Kibaha
ambao baadhi yao wameshindwa kutimiza ndoto zao kutokana na kukosa
elimu ya ujasiriamali hivyo ana imani kituo hicho kitaweza kusaidia kwa
kiasi kikubwa kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kwa wanawake
pamoja na jamii yote kwa ujumla.
Naye
Mkurugenzi wa Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Purple Planet ya Jijini
Dar es Salaam inayojishughulisha na kuwasaidia katika kuendesha
biashara zao na kuwainua kiuchumi wanawake wajasiriamali Hilda Kisoka
amebainisha kuwa mikakati yao waliyojiwekea ni kufika mbali zaidi na
kuuza bidhaa wanazozizalisha hapa nchini hadi nje ya nchi kwa lengo la
kujitangaza zaidi.
Alisema
kwamba ana imani wanawake wengi hapa nchini wana uwezo mkubwa wa
kuengeneza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu hivyo ameiomba serikali ya
awamu ya tano kuwasaidi kwa hali na mali ili kuweza kufika mbali katika
kuleta ushindani zaidi wa masoko katika nchi zingine za nje na
kuondokana na kuwa tegemezi.
Mkuu
wa Wilaya ya Kisarawe kulia Happiness Seneda akionyeshwa eneo lililopo
kata ya Mwendapole na Mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya Namelok Janet
Mwasuka wa kushoto ambapo kutajengwa kituo maalumu cha elimu kwa ajili
ya wasicahna na wanawake wajasiriamali waliopo Wilayani Kibaha Mkoani
Pwani (PICHA NA VICTOR MASANGU)
Mkuu
wa Wilaya ya Kisarawe kulia Happiness Seneda kulia akiwa amemshika
mmoja wa watoto huku akisikiliza maelekezo kuhusina na ujezni wa kiutuo
hicho maalumu cha elimu kwa ajili ya wasichan na wakinamama
kinachijengwa katika kata ya Mwendapole Wilayani Kibaha, kushoto kwake
ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Namelok Janet Mwasuka.
Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Nameloc akoinyesha eneo ambalo
kutajengwa kituo maalumu cha elimu kwa ajili ya wasichana na wanawake
wajasiriamali katika kata ya Mwendapole Wilayani Kibaha Mkoani Pwani
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...