Jeshi la
Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)
linasikitika kutangaza kifo cha Brigedia
Jenerali Albert Costantino Frisch (mstaafu) kilichotokea tarehe 13 Aprili 2017.
Marehemu Brigedia Jenerali Albert Costantino Frisch
(mstaafu) alizaliwa tarehe 13 Novemba
1944, mtaa wa Uhuru, Tarafa ya Kariakoo,
Wilaya ya Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam.
Alisoma na kuhitimu Shule ya Msingi mkoani Dar es Salaam na baadaye
kuendelea na masomo ya Sekondari katika Shule ya Sekondari St. Joseph Convert
School, Dar es Salaam hadi alipohitimu Kidato cha Nne mwaka, 1963.
Marehemu Brigedia Jenerali Albert Costantino Frisch
(mstaafu), alijiunga na JWTZ tarehe 07 Desemba 1964 na kutunukiwa Kamisheni
tarehe 22 Juni 1967. Alistaafu Utumishi Jeshini
kwa Heshima tarehe 30 Juni 1999.
Katika utumishi
wake Marehemu alishika Nyadhifa mbalimbali Ikiwemo Mkaguzi Mkuu wa Jeshi Makao
Makuu mpaka anastaafu.
Mwili wa Marehemu unatarajiwa
kuagwa rasmi tarehe 20 Aprili 2017 katika Hospitali ya Jeshi Lugalo kuanzia saa
10:30 Asubuhi.
MUNGU
AILAZE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU
BRIGEDIA
JENERALI ALBERT COSTANTINO FRISCH (MSTAAFU)
AMINA
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P
9203, Dar es Salaam, Tanzania.
Kwa Mawasiliano zaidi: 0756-716085.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...