Washindi wa shindano la kupiga picha wakiwa mbugani kutangaza utalii wa ndani wakiwa wameongoza na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya utalii Tanzania(TTB) ,Devotha Mdachi (katikati) wakiwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JNA Dar es Salaam kwa ajili ya Safari ya kuelekea Ngorongoro  na Serengeti kujionea vivutio zaidi ili kuweza kuwavutia watanzania wengine kutembelea vivutio hivyo.
 Washindi wa shindano hilo wakiwa na wenza wao wakijadili jambo kabla ya kuondoka na ndege ya shirika la ndege nchini Air Tanzania kuelekea katika mbuga za wanyama za Ngorongoro na Serengeti,ikiwa ni moja ya sehemu ya Safari zilizoratibiwa na bodi ya utalii nchini (TTB) kwa ajli ya kuhamasisha utalii wa ndani kwa Watanzania
Afisa uhusiano wa Bodi ya utalii Tanzania  akizungumza jambo na washindi wa shindano la kutuma picha kwa wapenzi ambao walishawahi kutembelea mbuga za wanyama ambao walipata kushinda tena fursa ya kutemmbelea Mbuga ya Ngorongoro na Serengeti.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...