Jovina Bujulu –MAELEZO

Ubora na thamani ya lugha ya Kiswahili duniani unadhihirika kwa kukubalika kwake,  hali hii inayopelekea lugha adhimu ya Kiswahili kuendelea kukua na kutumika katika nchi mbalimbali duniani kijamii, kiuchumi na hasa kibiashara na ushirikiano wa kimataifa.
Mchango wa lugha hii inaipa hadhi kubwa nchi yetu ambayo ni kitovu cha lugha hii inayotumika kama lugha rasmi ya mawasiliano katika nyanja mbalimbali na pia ndiyo lugha unganishi inayotumiwa na watu wengi nchini.
Kihistoria, lugha ya Kiswahili imekuwa na mchango mkubwa kutokana na kutumika katika harakati za ukombozi  na pia kuwaunganisha Watanzania na kuwafanya wawe wamoja.
Mara baada ya Uhuru Tanzania ilianzisha Baraza la Kiswahili (BAKITA) na kupewa jukumu la kuimarisha na kueneza lugha hii , pia kuhakikisha inatumika kwa ufasaha pamoja na kukuza msamiati wake ili iweze kukidhi matumizi yake.
Mwaka 1968, lugha hii ilianza kutumika  kufundishia katika shule za msingi hapa nchini. Hatua hii ilimaanisha kila mwanafunzi wa shule ya msingi kuifahamu vizuri kwa kuiandika, kuisoma na kuielewa.
Aidha, historia ya kuikuza na kuieneza lugha hii imeanzia mbali, mwaka 1962 hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliitumia kuhutubia Bunge la Tanganyika, baada ya utawala wake, Rais aliyemfuatia, Ali Hassan Mwinyi aliendeleza matumizi ya Kiswahili katika shughuli mbalimbali za mawasiliano.
Naye Rais wa Awamu ya Tatu, Mhe.Benjamin Mkapa na Rais wa Awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete walifanikisha maendeleo ya lugha hii kwa kuhimiza matumizi fasaha katika nyanja za elimu, shughuli zote za Serikali, katika shughuli au mikusanyiko rasmi pamoja na matumizi mengine ya mawasiliano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...