MFUKO
wa uwekezaji wa pamoja wa UMANDE UNIT TRUST (UUT) leo umezindua rasmi
mpango-mkakati wake wa kifedha utakaowawezesha wawekezaji wadogo na wale
wenye kipato cha chini na cha kati waweze kununua hisa za kampuni ya
Vodacom Tanzania kwa kupitia njia ya vipande.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa
Kampuni ya CORE Capital Limited ambayo ndio iliyobuni mfuko huo, Bw
George Fumbuka alisema kiwango cha chini cha ununuzi wa hisa za Vodacom
ni 85,000/= (hisa 100 kwa 850/= kila hisa), kwa mkupuo kinaweza kuwa
kiasi kikubwa kwa wawekezaji wadogo wadogo, wa kipato cha chini.
“Mantiki
ya mkakati huu ni kuwakusanya pamoja wale wote wenye mitaji midogo ili
waweze kwa pamoja kufikia viwango vinavyohitajika katika ununuzi wa hisa
za VODACOM. Kima cha chini ni shilingi 13,500 tu, yaani vipande 100 vya
shilingi 135/= kila kimoja. Dhana hii si mpya kwa Watanzania; mara
nyingi tu hutumika kwenye shughuli za pamoja, huitwa “UMOJA NI NGUVU”.’’ Alisema
Alisema
mpango huo pia utatoa fursa kwa wawekezaji wa kigeni wakiwemo
watanzania wanaoishi nje ya nchi (diaspora) kuweza kunufaika na hatua
hiyo ya serikali kwa kuwa uuzwaji wa hisa hizo kupitia soko la Hisa la
Dar es Salaam (DSE) hautoi fursa kwa wawekezaji wa kigeni.
“Kwa
kuwa mauzo ya hisa hizo hapa nchini hayahusishi wawekezaji wa kigeni
wakiwemo watanzania wanaoishi nje yaani Diaspora, milango ipo wazi kwao
kupitia mfuko wa uwekezaji mtaji wa Umande (Umande’s capitalisation
fund),utakaowawesha kununua vipande badala ya wao kwenda moja kwa moja
kwenye soko la hisa,’’ alisema.
Zaidi
Bw Fumbuka aliwahakikishia walengwa wa mpango huo kuhusiana na uhakika
wa wao kujipatia gawio na faida zitokanazo na mtaji (dividends and
capital gains) kama kawaida kwa kuwa thamani ya vipande itakwenda
sambamba na thamani ya hisa za kampuni hiyo ya huduma za simu za
mkononi.
“Mpango
mkakati huu una baraka zote za Kampuni ya Vodacom na za Mamlaka ya
Masoko na Mitaji (CMSA) chini ya Kanuni za Mifuko ya Uwekezaji ya mwaka
1997.” Alibainisha.
Hata
hivyo alifafanua kwamba watakaopitia mkakati huo, wawe ni wawekezaji
wadogo wadogo au wale wa nje, hawataweza kumiliki hisa za VODACOM moja
kwa moja; badala yake watamiliki vipande vya Mfuko utakaopatikana kwa
michango yao.
“Kwa
maana hiyo Mfuko wa UUT ndiyo utanunua hisa za VODACOM kwa niaba yao na
watafaidi matunda ya uwekezaji kwa njia hiyo. ‘’ alisema huku akiongeza
kuwa Vipande vitanunuliwa kwa njia ya simu tu: *150*36#, huku kima cha
chini kikiwa ni Tsh 13,500/=.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya CORE Capital Limited ambayo ndio iliyobuni mfuko huo, Bw
George Fumbuka (katikati) akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam
leo mpango-mkakati unaoendeshwa na kampuni hiyo kupitia Mfuko wa uwekezaji wa
pamoja wa UMANDE UNIT TRUST (UUT) utakaowawezesha wawekezaji wadogo na wale
wenye kipato cha chini na cha kati waweze kununua hisa za kampuni ya Vodacom
Tanzania kwa kupitia njia ya vipande. Wengine ni Meneja wa Mfuko huo Bi Sandra Felician
na Naibu wake Bi Nkunde Shoo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...