Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa atafungua maonesho ya Mifuko ya Uwezeshaji wananchi kiuchumi yatakayofanyika mkoani Dodoma katika viwanja vya mashujaa kuanzia tarehe 18-22 April 2017. 

Akizungumza na waandishi wa Habari Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi(NEEC) Bi.Beng’i Issa amesema Maonyesho hayo yameandaliwa na Baraza hilo kwa lengo la kutoa elimu kwa umma juu ya huduma mbalimbali zitolewazo na mifuko yote ya uwezeshaji wananchi kiuchumi. 

“Tumeamua kufanya maonesho haya kwa mara ya kwanza kwa sababu changamoto kubwa tuliyonayo ni kuwa mifuko hii haifahamiki sana na wananchi, wengi walikuwa hawajui wafanye nini ili waweze kupata fursa ya kupata mitaji na kusaidiwa na mifuko hii ambayo imeanzishwa na Serikali kwa ajili yao”,Aliongeza Bi.Beng’i. 

Amesema maonyesho hayo yatawapa wananchi fursa ya kuonana na watu ambao wamefanikiwa katika kipindi kilichopita na hasa kujua jinsi gani watafaidika na mikopo ambayo inapatikana kupitia mifuko hii. 

Ameitaja mifuko ambayo itashiriki ni pamoja na Mfuko wa kuendeleza wajasiriamali wananchi, Mfuko wa Uwezeshaji wa Mwananchi, Mfuko wa Pembejeo za Kilimo , Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, Mfuko wa Dhamana za mikopo kwa wajasiriamali wadogo na wa kati na Mfuko wa Dhamana za Mikopo kwa Mauzo ya Nje ya Nchi. 

Mifuko mingine ni Mfuko wa kuwasaidia makandarasi,Mfuko wa Maendeleo ya Jamii,Mfuko wa Misitu Tanzania,SELF Microfinance Fund na PASS Trust Fund. 

Kauli mbiu ya Maonyesho haya ni “WEZESHA WANANCHI KIUCHUMI ILI KUJENGA UCHUMI WA KATI NA TANZANIA YA VIWANDA” 

 Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bi.Beng’I Issa akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) juu ya Maonesho ya Mifuko ya Uwezeshaji wananchi kiuchumi yatakayofanyika katika viwanja vya mashujaa kuanzia tarehe 18-22 April 2017.
 Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bi.Beng’I Issa akimsikiliza Mhasibu Mkuu kutoka Mfuko wa Rais wa kujitegemea Bw.Ahazi Kibona juu ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo.
Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bi.Beng’I Issa akizungumz ana waandishi wa Habari (hawapo pichani) juu ya Maonesho ya Mifuko ya Uwezeshaji wananchi kiuchumi yatakayofanyika katika viwanja vya mashujaa kuanzia tarehe 18-22 April 2017.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...