Katibu Mkuu wa Yanga Chrles Mkwasa.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Kuelekea mechi ya marudiano ya mchezo wa hatua ya mtoano wa Kombe la Shirikisho baina ya wawakilishi wa Tanzania  klabu ya soka ya Yanga na Mc Alger ya Algeria imeweka wazi kikosi cha wachezaji 20 watakaoondoka kesho kueleo nchini Algeria.

Yanga wanatarajiwa kuondoka kesho majira ya saa 12 jioni kuelekea nchini Algeria ambapo watacheza na MC Alger siku ya Jumamosi katika Jiji la Alger.

Akitaja kikosi hicho, Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa amesema kuwa wachezaji wapo tayari kwa ajili ya kwenda kupambana nchini Algeria na tunafahamu ni mchezo mgumu lakini pia ni muhimu sana kwao wakihitaji ushindi wa aina yoyote au sare ili kusonga mbele na kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.

Mkwasa amesema kuwa anapenda kuwa msafara wa wachezaji 20, benchi la ufundi na viongozi utaondoka kesho jioni majira ya saa 12 kwa ndege ya shirika la Emirate kupitia Dubai.

Wachezaji watakaondoka ni Makipa; Deogratius Munishi na Beno Kakolanya . Nafasi ya ulinzi ni ; Nadir Haroub , Vicent Bossou , Juma Abdul , Vicent Andrew, Oscar Joshua , Juma Abdul , Mwinyi Haji, Hassan Kessy na Kelvin Yondani. 

Nafasi ya viungo ni; Thabani Kamusoko, Haruna Niyonzima, Deusi Kaseke,Said Makapu, Juma Mahadhi, Saimoni Msuva, Geofrey Mwashuiya na Emmanuel Martin.
 Upande wa washambuliaji ni Amissi Tambwe na Donald Ngoma

Wachezaji wafuatao wataukosa mchezo huo kwa sababu mbalimbali ambao ni Justine Zulu, Malimi Busungu, Matheo Antony, Ally Mustapha, Pato Ngonyani, Obrey Chirwa na Yusuph Mhilu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...