na wale wote wenye nasaba na
Tanzania waishio Leicester na vitongoji vyake kuwa Balozi wa Tanzania nchini
Uingereza Dk. Asha-Rose Migiro anatarajia kufanya ziara ya mjini Leicester Jumamosi ya
tarehe 22 Aprili 2017.
Katika ziara hiyo Mh. Balozi
Migiro atapata fursa ya kuongea
na Watanzania wote na pia kutembelea shughuli mbalimbali za kimaendeleo
zinazofanywa na wajasiriamali wa Kitanzania waishio Leicester. Ziara hii pia
utawawezesha watanzania kumpatia Mhe. Balozi mawazo,
maoni na ushauri kuhusu masuala
mbalimbali yenye maslahi kwa wanadiaspora na Serikali yetu kwa ujumla.
Mkutano utafanyika kuanzia saa
nane kamili mchana kwenye ukumbi ufuatao:
Peepul Centre,
Orchardson Avenue,
Leicester,
LE4 6DP
Tunaomba Watanzania wote
mjitokeze kwa wingi kumkaribisha Balozi wetu na kushiriki katika mazungumzo
yatakayosaidia kuharakisha maendeleo ya
wanadiaspora na nchi yetu. Kuja kwenu ndio kufanikisha
ziara hii muhimu. Tafadhali mjulishe mwenzio.
Asanteni kwa ushirikiano wenu.
JUMUIYA YA WATANZANIA LEICESTER
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...