NA ALLY DAUD-WAMJW DODOMA

ASILIMIA 24.9 ya watanzania huvutishwa moshi wa tumbaku katika sehemu za kazi hivyo kuchangia kuongezeka kwa wagonjwa wa saratani nyingi hapa nchini.

Hayo yamebainishwa kwenye taarifa iliyotolewa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu inayohusu Maadhimisho ya siku ya kutotumia tumbaku duniani.

“Hali hii isipodhibitiwa vifo vitaongezeka kufikia asilimia 80 kwenye nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania na milioni 8 kwa mwaka duniani kote ifikapo 2030” iliongeza taarifa hiyo.

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa katika uchunguzi uliofanywa mwaka 2013 na Wizaya ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia Taasisi ya Utafiti wa Maradhi ya Binadamu(NIMR) wakishirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) ulionyesha asilimia 24.9 huvutishwa moshi wa tumbaku sehemu za kazi, asilimia 14 ya watanzania hutumia tumbaku na asilimia 17 ya watanzania hawavuti lakini wanavutishwa moshi wa tumbaku.

Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa tumbaku inaua watu takribani milioni 6 kila mwaka na moshi wake huua zaidi ya watu laki 6 ambao sio wavutaji wa tumbaku duniani .

Mbali na hayo Wizara ya afya imedhamiria kupiga vita matumizi ya tumbaku kwa kuhakikisha hakuna matangazo ya tumbaku kyupitia kwenye mabango barabarani,luninga,redio,sinema,au kubandikwa ukutani na kwenye magari ya matangazo.

Madhimisho ya Siku ya kutovuta Tumbaku huadhimishwa Mei 31 kila mwaka duniani kote na kwa mwaka huu imebeba kauli mbiu isemayo”TUMBAKU-TISHIO KWA MAENDELEO” .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...