Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Asha-Rose Migiro alifanya ziara ya kuwatembelea watanzania waishio Reading na Bekshire tarehe 6/5/2017. Wakati wa ziara hiyo Mhe. Balozi Migiro alipata fursa ya kufanya mkutano na kuwatembelea baadhi ya watanzania hao kwenye maeneo yao ya kazi.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Asha-Rose Migiro akiwa pamoja na baadhi ya wana diaspora waishio Reading na Bekshire waliohudhuria mkutano.
 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mhe. Asha-Rose Migiro akisalimiana na Bw. Daniel Samwenda mmoja wa wamiliki wa kampuni ya McDaan Finance inayojishughulisha na shughuli mbali mbali za kifedha kama kutoa mikopo ya muda mfupi.
 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Asha-Rose Migiro akipata maelezo kutoka kwa Bw. Hassan Abdula Mkurugenzi wa Kampuni ya Hill View Family Co. Ltd inayojishughulisha na usafirishaji wa mizigo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...