Balozi Mteule wa Tanzania nchini India, Baraka Luvanda akiongea akipokea Kitabu cha maswala ya Uwekezaji kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Clifford Tandari wakati Balozi huyo alipotembelea kituo hicho, Balozi Luvanda ameiomba TIC iweze kushirikiana naye ili kuweza kuongeza idadi ya Wawekezaji wa India nchini Tanzania kwenye sekta mbalimbali kama Afya, viwanda na Utalii. Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji amesema India ni mshirika mkubwa wa Tanzania katika Uwekezaji na moja kati ya nchi tano bora zenye uwekezaji mkubwa hapa nchini na kumuomba Balozi Luvanda kuhakikisha anajitahidi kutangaza fursa zaidi za Uwekezaji zilizopo hapa nchini ili uwekezaji uwe na manufaa kwa maeneo mengi zaidi ya nchi.
Balozi Mteule wa Tanzania nchini India, Baraka Luvanda (wa pili kushoto) akipata maelezo mafupu kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Clifford Tandari (kulia) wakati Balozi huyo alipotembelea kituo hicho jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...