Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imetoa mafunzo kwa watumishi wote wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida juu ya alama zinazopatikana katika noti halali za fedha ya Tanzania leo asubuhi katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa. 

Akitoa mafunzo hayo Afisa Kutoka Benki Kuu ya Tanzania Rehema Zongo amewafafanulia watumishi hao namna ya kutambua noti halali kwa vitendo huku akisisitiza alama muhimu zinazopatikana katika noti halali ili waweze kutofautisha na zile bandia.

Zongo amesema watumishi wanatakiwa kuichunguza noti halali, waipapase ili kuhisi mparuzo kwenye maneno yaliyoandikwa kwa maandishi maalumu mfano maandishi yanayoeleza fedha halali kwa malipo ya shilingi mia tano, elfu moja, elfu mbili, elfu tano na elfu kumi.

Amewasisitizia kuwa wanaweza kuitambua noti halali kwa kuangalia sura ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere inayoonekana unapoimulika noti kwenye mwanga na pia kukagua utepe maalumu kwenye noti za shilingi 500, 1000, 2000, 5000 na 10,000 unaoonekana kama madirisha yenye umbo la almasi ambapo hubadilika badilika noti inapogeuzwa geuzwa. 
Afisa Utumishi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Justo Herman akikagua noti halali wakati wa mafunzo yaliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania.
Mwangalizi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida Khadija Hamisi na Mkaguzi wa ndani Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Alfred Kalama wakisikiliza kwa umakini alama zinazopatika katika noti halali wakati wa mafunzo yaliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania.
Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida George Kulwa akitoa shukrani kwa niaba ya watumishi wote waliopata mafunzo ya Benki kuu ya Tanzania.
Maafisa kutoka Benki Kuu ya Tanzania Rehema Zongo na Rajab Ibrahimu wakisikiliza maswali na kutoa ufafanuzi kwa watumishi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa mara baada ya kutoa mafunzo ya alama za noti halali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...