Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Simba, Zacharia Hans Poppe ameachia ngazi.
Habari za uhakika zimeeleza kuwa Hans Poppe ameandika barua ya kuachia ngazi kwa madai kuwa anaona mambo yanaendeshwa ndivyo sivyo.
Chanzo chetu cha kuaminika kinaeleza kuwa "Hans Poppe ameachia ngazi kwa kuwa hakufurahishwa na mlolongo ulivyokuwa hadi Simba kuingia mkataba wa SportPesa,” kilieleza chanzo.
"Hans Poppe ameandika barua kujiuzulu kwenye kamati ya utendaji, maana yake anaondoka moja kwa moja katika nafasi ya mwenyekiti wa kamati ya usajili.
"Kilichomchukiza, anasema kuna kundi lililoongozwa na Rais Evans Aveva na makamu Geofrey Nyange Kaburu, lilifanya mambo kimya kimya na Hans Poppe amesema hata Mo Dewji aliyeisaidia Simba mishahara naye hakushirikishwa hata kiungwana tu, hivyo amepinga hilo."
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...