Taarifa iliyoifikia Globu ya Jamii  inaeleza kuwa leo saa tatu asubuhi imetokea ajali katika eneo la Rhotia Wilaya ya  Karatu Mkoani Arusha, iliyohusisha Basi lililokuwa limebeba wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya St Lucky ya jijini Arusha, inayodaiwa kuwa ilipoteza mwelekeo na kupindukia korongoni wakati wakiwa safarini kuelekea Karatu waliokuwa wakienda kufanya mitihani ya ujiranimwema na wanafunzi wenzao wa Shule ya Tumaini English Medium ya mjini Karatu.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Arusha,  Afande Charles Mkumbo, wanafunzi 32 , walimu 2 na dereva wa gari hilo wamepoteza maisha huku wanafunzi  wengine 4 na mtu mzima mmoja  wakiwa wamejeruhiwa.
Chanzo cha ajali hiyo mbaya kutokea mkoani humo bado haijajulikana na uchunguzi unaendelea. Globu ya Jamii inatoa rambirambi kwa wafiwa na kuwatakia majeruhi nafuu ya haraka. 
Zoezi la uokoaji likiendelea.

 Umati wananchi ukiwa katika nje ya chumba cha maiti cha hospitali ya Mount Meru jijini Arusha kutambua miili ya wanafunzi na wanafunzi waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo.
 Umati wananchi ukiwa katika nje ya chumba cha maiti cha hospitali ya Mount Meru jijini Arusha kutambua miili ya wanafunzi na wanafunzi waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...