Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akikagua jengo la kituo cha Polisi kata ya Iselamagazi ambalo limejengwa kwa nguvu za wananchi wakishirikiana na mbunge wao wa Solwa Ahmed Salimu.

Ukaguzi wa jengo ukiendelea
Mkuu wa wilaya Josephine Matiro akiteta jambo na viongozi wa serikali pamoja na baadhi ya madiwani wa halmashauri kabla ya kuingia kwenye mkutano wa viongozi wa Sungusungu na watendaji wa vijiji,kata na vitongoji kujadili ajenda mbili za ulinzi na usalama pamoja na kuunda ushirika wa vyama vya kuuza mazao ili kuinua wakulima kiuchumi sambamba na kuhifadhi chakula cha akiba ili kukabiliana na janga la njaa hapo baadae.
Mkuu wa wilaya Josephine Matiro akizungumza na viongozi wa Sungusungu,baadhi ya watendaji wa kata ,vijiji,vitongoji na Madiwani wa halmashauri hiyo juu ya kudhibiti uhalifu kwenye tarafa hiyo ya Nindo pamoja na kuwafichua wahalifu ambao huhatarisha hali ya amani. 




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...