Mamia ya wakulima wanamiminika kwenye duka dogo la pembejeo lilipo Mafinga mkoani Iringa kupeleka mazao yao kwa ajili ya kupata utatuzi. Bwana shamba wa kampuni ya Yara Tanzania Ltd Bw. Andrew Mwangomile bila kuchoka amekuwa akiwaelezea wakulima walioleta mahindi yao kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi wa changamoto zao.
Bwana shamba huyo alipohojiwa aliesema, Yara Tanzania tumeandaa huduma maalumu inayoitwa "crop clinic day" (siku ya zahanati ya mimea) huduma hii inafanana na ile binadamu au kiumbe hai yeyote anapohitaji huduma ya kwanza akijisikia kuumwa ili kupata huduma ya kwanza. Kwenye siku hii maalumu wakulima huleta mizizi, majani au zao lenyewe kwa ajali ya bwana shamba kuweza kumsaidia kutatua kwa haraka tatizo linalokabili mmea huo."   
'Moja ya kauli mbiu zetu ni mkulima afanikiwe na kuweza kulisha dunia kwa kutoa huduma muhimu zinazoweza kumsaidia mkulima kuzalisha mazao bora na sio bora mazao. Yara Tanzania inahakikisha ili mpango huo utekelezeke ni kusaida wakulima kutatua changamoto mbali mbali ya mazao. 
"Siku ya zahanati kwetu ni muhimu na tunatoa huduma hii Bure kwenye mikoa yote nchini kushikiana na mawakala wadogo na wakubwa", aliongeza bwana shamba huyo  alipohojiwa kwa njia ya simu afisa masoko na mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Linda Byaba 
Wakulima wakipata maelezo yaliopo kwenye kipeperushi cha mahindi cha Yara Tanzania kutoka kwa Bw. Andrew Mwangomile  baada ya zao lake kugundulika na changamoto kadhaa hanani ya mimea ilitolewa
 Bwana Shamba Andrew Mwangomile akielezea aina ya virutubisho vinavuohitajika kwenye zao la mahindi na vinavyopatikana kwenye mbolea aina ya YaraMila CEREAL
 Afisa Ugani wa Yara Tanzania Andrew Mwangomile akiwaelezea wakulima waliotembelea kwenye duka la pembejeo lengo la Zahanati ya mimea iliyoanzishwa na Yara Tanzania kwa kutumia mfano wa zao la mahindi
 Picha ya zao la mahindi lililoletwa na mkulima kwa ajili ya uchunguzi siku ya zahanati ya mimea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...