Na Anil Ricco , Globu ya Jamii

Mkuu wa Jeshi la polisi Nchini (IGP),Simon sirro ameahidi kutoa sh.milion 10 kwa yeyote atakayetoa taarifa za kufanikisha kuwakamata watu wanaofanya mauaji ya viongozi huko Kibiti wilayani Rufiji Utete mkoani Pwani.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Sirro amesema kumekuwa na mauaji ya wananchi na Askari katika Wilaya ya Rufiji Utete pamoja na Wilaya ya Mkuranga ambayo yamekuwa yakifanywa na wahalifu wachache kwa malengo wanayoyajua wao,

Amesema Jeshi la Polisi bado linaendelea na Operesheni mbalimbali kuhakikisha kwamba vitendo hivyo haviendelei kuweza kubaini mzizi.

Aidha Mkuu wa Jeshi la Polisi Mpya amezungumzia juu ya waendesha boda boda kuwa na tabia ya kukaidi kufata sheria za usalama barabarani ikiwemo kubeba abiria zaidi ya mmoja ‘mishikaki.

Sirro amesema waendesha bodaboda wanashindwa kufuata sheria za usalama barabarani kwa kupita taa nyekundu pamoja na kutovaa kofia ngumu ‘Helment’ ambapo kumesababisha wengine vifo na majeruhi ya kuwafanya kuwa na ulemavu wa kudumu .

Hata hivyo amesema kumekuwa na malalalamiko dhidi ya baadhi ya Askari polisi kujihusisha na vitendo vya rushwa lakini pia baadhi ya wananchi kuwashawishi Askari kupokea rushwa ikiwa ni sehemu ya ngao ya kukwepa kuwajibishwa pindi wanapokuwa wamefanya makosa.
Sehemu ya waandishi wa habari pamoja na Makamanda wa Jeshi la Polisi wakimsikiliza IGP Mpya, Simon Sirro alipokuwa akizungumza na Wanahabari mapema leo jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.
Mkuu wa jeshi la polisi Nchini (IGP),Simon sirro akizungumza na waandishi habari (hawapo pichani) juu ya hatua mbalimbali za kuweza kudhibiti masuala ya uhalifu likiwemo la mauaji yanayoendelea Kibiti leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...