Bongolos ni kundi la wanamuziki wawili, Drew (Kiume) na Tamu (Kike), lenye makazi yake jijini Dar es Salaam, Tanzania. Bongolos ni kundi lililoundwa na mtayarishaji mkongwe wa muziki Afrika Mashariki P-Funk Majani ndani ya Bongo Records mwaka 2016. Jina Bongolos lilipatikana kutoka kwa mwanamuziki wa hip hop wa Marekani, Mims baada ya kuja kufanya kolabo nchini Tanzania chini ya Bongo Records.

Drew wa Bongolos alikutana na mtayarishaji P-Funk Majani baada ya kuona ujumbe mfupi wa maneno kwenye mitandao ya kijamii kwamba mtayarishaji huyo alikuwa anatafuta wanamuziki chipukizi. Tamu wa Bongolos alikutana na mtayarishaji huyo baada ya kuunganishwa na rafiki yake.
Bongolos wanafanya muziki ambao ni mchanganyiko wa muziki wa kufoka na kuimba ambao pia unawezwa kuitwa Bongo Flava. Muziki wao umejawa na vionjo vya Kiafrika kwenye mirindimo yake. Bongolos wameachia ngoma yao ya kwanza iitwayo Wape.


Song : WAPE



Artists : Bongolos ft Asteria Mvungi


Music Producer : P-Funk Majani


Copyright Holder : Bongo Records Ltd

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...