Naibu Waziri wa Nchi,Ofisi ya
Rais, Tamisemi Selemani Jafo amewapongeza viongozi wote pamoja na
wananchi wa wilaya ya kisarawe katika ujenzi wa zahanati Mpya 11 pamoja
na wodi 2 za wazazi.
Jafo ambaye pia ni Mbunge wa
Jimbo la Kisarawe alitoa pongezi hizo alipokuwa akifanya ukaguzi wa
miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni Kisarawe.
Ujenzi huo unafanyika kupitia
fedha za mfuko wa jimbo ambazo zimetumika kununua saruji na mabati na
pia fedha kutoka Halmashauri ya wilaya ya kisarawe na michango ya
wananchi.
Akiweka jiwe la msingi katika
ujenzi wa zahanati ya visiga, Jafo alipongeza wananchi wa visiga kwa
kuunga mkono juhudi ya serikali ya awamu ya tano katika kujileta
maendeleo.Aliwaomba viongozi wote waendelee na moyo huo huo wa mshikamano ili kufanikisha utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2015.
Katika hatua nyingine, Wananchi
wa Tarafa ya Chole wilayani Kisarawe wameishukuru serikali ya awamu ya
tano baada ya Mbunge wa jimbo la Kisarawe na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi
ya Rais Tamisemi kukabidhi gari la wagonjwa aina ya Toyota Landcruiser
kwa Kituo cha Afya chole.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa Tarafa ya Chole katika kituo cha Afya Chole.
Gari la wagonjwa lilokabidhiwa katika Kituo cha Afya cha Chole
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Kituo cha Afya Chole pamoja na viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe mara baada ya Kukabidhi gari la wagonjwa.
Jengo la Zahanati ya Visiga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...