NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo amewataka wakandarasi wanaojenga miradi ya miundombinu mbalimbali kwenye Halmashauri nchini kuhakikisha miradi hiyo inakamilika ndani ya muda na inakuwa na ubora unaotakiwa.

Jafo alitoa kauli hiyo leo katika uzinduzi wa mradi wa Maji Wilunze wilayani humo.

Mradi huo umefanikiwa kukamilika na kuzinduliwa rasmi kufuatia maagizo aliyoyatoa Machi,26 mwaka huu baada ya kutembelea na kubaini kuna uzembe Mkubwa katika utekelezaji wa mradi huo.

Baada ya kubaini hilo, Jafo alitoa kalipio kwa watendaji wa Halmashauri pamoja na Mkandarasi wa ujenzi wa mradi na kuagiza mradi huo ukamilike haraka ifikapo leo Mei 30, mwaka huu, kinyume cha hapo atawachukulia hatua kali watendaji na Mkandarasi endapo angeshindwa kukamilisha ndani ya muda huo.

Aidha, Jafo alimwambia mkandarasi wa Mradi huo kuwa endapo asipotekeleza asitegemee kupata kazi yeyote iliyo chini ya Halmashauri yeyote hapa nchini kwani Ofisi ya Rais Tamisemi haiwezi kuvumilia wakandarasi wazembe. 
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo pamoja na Mbunge wa Jimbo la Chilonwa Joel Mwaka wakipiga makofi baada ya kuzindua mradi wa maji Wilunze.
Jiwe la msingi la Mradi wa maji Wilunze
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akizungumza mara baada ya kumtwisha ndoo ya maji mmoja wa wananchi wa kijiji cha Wilunze.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...