Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma, akisalimiana na baadhi ya Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Hanang/Katesh pindi alipowasili katika Mahakama hiyo kwa lengo la kujionea hali ya utoaji haki nchini.
 Kaimu, Jaji Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma akiongea na Watumishi wa Mahakama ya Wilaya Hanang, kushoto ni Kaimu Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha, Mhe. Sekela Moshi.
 Watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Hanang wakimsikiliza Kaimu Jaji Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma alipokuwa akizungumza nao alipofika Mahakamani hapo kwa lengo la kujionea hali ya utendaji kazi wa Mahakama hiyo.
 Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Joel Bendera pindi alipomtembelea ofisini kwake mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Joel Bendera (kushoto) akimueleza jambo Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania pindi alipomtembelea ofisini kwake mkoani Manyara, katika maongezi yake Mkuu wa Mkoa huo, ameisifu Mahakama mkoani humo kwa kusaidia kupunguza mgogoro kati ya Wakulima na Wafugaji Wilayani Kiteto mkoani humo kufuatia maamuzi yaliyotolewa na Mahakama kuhusiana na mgogoro huo.

Kwa upande wake Kaimu Jaji Mkuu amepongeza ushirikiano uliopo kati ya Serikali ya Mkoa na Mahakama na kusisitiza muendelezo wa ushirikiano huo kwa manufaa ya wananchi. (Picha na Mary Gwera)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...