Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma akisamiliana na Watumishi wa Mahakama, Kanda ya Arusha alipowasili katika viwanja vya Mahakama Kuu-Arusha kukamilisha ziara yake ya siku mbili mkoani humo. A
Kaimu Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha,Mhe. Kamugisha akimsomea taarifa ya hali ya utendaji kazi wa Mahakama katika mkoa huo. Lengo la ziara ya Mhe. Kaimu Jaji Mkuu katika Kanda hiyo ni kujifunza na kuona hali halisi ya mazingira ya kazi na utekelezaji wa majukumu.
 A 1
Naibu Msajili, Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha, Mhe. Rumisha (wa kwanza kulia) akimuonesha Mhe. Kaimu Jaji Mkuu, moja ya kumbi za Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha pindi alipokuwa akikagua ofisi mbalimbali za Mahakama ya Mkoa na Mahakama Kuu katika Kanda hiyo.
 A 2
Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Juma akiwa katika Kompyuta Mpakato akikagua Mfumo wa Kuratibu takwimu za Mashauri kwa njia ya Kielektroniki (JSDS) kuhakikisha kama inafanya kazi ipasavyo, pembeni ni Afisa TEHAMA, Mahakama Kuu-Kanda ya Arusha, Bw. Athuman
 A 4
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, akiongea na Mahakimu na Watumishi wengine wa Mahakama (hawapo pichani), katika maongezi yake na Watumishi hao Mhe. Jaji Prof. Juma amewataka na kuwasisitiza Watumishi hao kufanya kazi kwa kuzingatia Maadili ikiwa ni pamoja na kuwa na lugha nzuri kwa Wateja/Wananchi wanaowahudumia. kulia ni Kaimu Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Kanda ya Arusha na kushoto ni Mhe. Rumisha, Naibu Msajili-Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...