Kampuni ya bia ya Serengeti Brewaries Ltd (SBL), imezindua bia mpya aina ya Lite, ikiwa ni muendelezo wa bia mama ya Serengeti Premium Lager.
 
Akizungumza na waandishi wa Habari, wakati wa uzinduzi wa bia hiyo, mkurugenzi wa fedha na bodi ya SBL, Kalpesh Mehta, amesema bia hiyo itakayokwenda kwa jina la Serengeti Premium Lite inazalishwa kwa kutumia utaalamu wa kisasa.

Aidha bia hiyo ina ladha kamili ambayo burudani yake ni zaidi ya bia zote za aina ya Lite ambazo kwa sasa zipo sokoni.Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, bia hiyo inauzwa sh.1500 kwa chupa na kwamba inatarajiwa kuteka soko na jumuiya ya wanywaji wake ambao kwa kipindi kirefu wamekuwa wakitafuta bia halisi ya kitanzania.

Ameongeza kuwa, Bia hiyo mpya haina sukari kwa hiyo itakuwa ni chaguo zuri kwa wale wote wasiotumia sukari."Huu ni mwitikio wa wateja wetu ambao wamekuwa wakiitafuta bia ya aina hii kwa muda mrefu"

"Tunaamini kuwa bia hii Ya Serengeti Premium Lite, ambayo imebuniwa na kutengenezwa na wazalishaji bia (bremaster), wa kitanzania kwa watanzania, itawaleta wateja wetu pamoja zaidi kadri watakapokuwa wakifurahia urithi wetu wa amina hii ya bia", amesema Mehta.

Ameongeza kuwa, bia hiyo ya Premium Lite ina ubora wa kimataifa sawa na bia mam ya Serengeti Premium Lager ambayo nimepokea zaidi ya medalist 10 za ubora wa kitaifa na kimataifa.

 Mkurugenzi wa Fedha na Bodi ya SBL ,Kalpesh Mehta akizungumza na waandishi wa Habari juu ya uzinduzi wa bia mpya ya Serengeti ya sh.1500 katika ukumbi wa Serena Leo jijini Dar es salaam,kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko, Ceaser Mloka kulia ni Anitha Lwehumbiza
Mkurugenzi wa Masoko, Ceaser Mloka akizungumza na waandishi wa Habari juu ubora wa bia iliyozinduliwa ya Serengeti ya sh.1500 Leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...