Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Leonard Chamuriho amewakumbusha wadau wa usafiri wa anga kusughulikia na kumaliza tatizo la wizi na udokozi katika usafiri wa anga, hali ambayo amesema inahatarisha usalama na ustawi wa sekta hii hapa nchini.

Katika hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa 42 wa kamati ya Kitaifa ya Uwezeshaji Usafiri wa Anga (National Air Transport Facilitation Committee) iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchukuzi - Sekta ya Uchukuzi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Rogatus Hussein Mativila, Dkt. Chamuriho ametoa mfano wa taarifa za hivi karibuni katika vyombo vya habari kuhusu wizi wa mafuta ya ndege hali ambayo amesema itajenga hofu kwa watumiaji wa uchukuzi wa anga . 

"Matukio kama haya hayaatarishi usalama tu, lakini pia ustawi wa sekta kwa vile yatajenga hofu kwa wasafiri na kusababisha wachague njia nyingine". Alisema Katibu Mkuu na kuongeza ustawi wa usafiri wa anga katika nchi yoyote, unategemea na upatikanaji wa huduma bora katika viwanja vya ndege, usalama wa abiria na mali zao, ndege na miundombinu mbali mbali .
Kaimu Mkurugenzi Udhibiti Masuala ya Kiuchumi , Mamlaka ya Usafiri wa Anga Dan Malanga (wa kwanza Kushoto) akimsikiliza Meneja wa uwanja wa ndege wa Dodoma, Julius K. Mlungwana,(wa Pili Kushoto) wakati kamati ya kitaifa ya Uwezeshaji Usafiri wa Anga ilipotembelea kiwanja cha ndege Dodoma May, 8 2017.
Kaimu Mkurugenzi Udhibiti Masuala ya Kiuchumi, Mamlaka ya Usafiri wa Anga, Dan Malanga (Amesisima) akisisitiza jambo wakati wa kikao cha 42 cha wajumbe wa kamati ya kitaifa ya Uwezeshaji Usafiri wa Anga kilichofanyika ukumbi wa Hazina mjini Dodoma May, 8 2017.
Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchukuzi, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Rogatus Hussein Mativila akifungua kikao cha 42 cha wajumbe wa kamati ya Kitaifa ya Uwezeshaji Usafiri wa Anga Kilichofanyika Ukumbi wa Hazina mijini Dodoma May, 8 2017.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...