Katibu
Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Ndugu Abdrahamani Kinana yuko nchini
Angola akiongoza ujumbe wa CCM katika kikao cha Makatibu Wakuu wa Vyama
vya ukombozi wa kusini mwa Afrika( Front Line State parties). Pia
Ndugu Katibu Mkuu ameongoza Majadiliano na vyama Rafiki vilivyoshiriki
Mkutano huo kikiwemo Chama Cha Kikomunisti Cha watu wa China .
Ujumbe
wa CCM ambao umejumuisha katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi( Ndg.Humphrey
Polepole) Katibu wa Siasa na Uhusiano wa kimataifa Ndg. Ngemela Lubinga na watendaji wa Jumuiya za Chama hicho katika mazungumzo na ujumbe wa Chama Cha Kikomunisti Cha watu wa China nchini Angola. Vyama rafiki vimepongeza CCM mpya na mwenendo wake.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kushoto) akizungumza jambo na baadhi ya viongozi wa vyama Rafiki vilivyoshiriki
Mkutano huo kikiwemo Chama Cha Kikomunisti Cha watu wa China nchini Angola.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...