Hussein Makame, NEC-aliyekuwa Dodoma 

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa kura zilizoharibika zinazopatikana kwenye chaguzi zinasababishwa na wapiga kura wengi kukosa elimu ya mpiga kura.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo Bw. Kailima Ramadhani wakati akijibu swali la mmoja wa watangazaji wa kituo cha Redio AFM cha mkoani Dodoma katika mfululizo wa kutoa elimu ya mpiga kura kupitia vituo vya redio.

Mtangazaji huyo alihoji kwa nini inajitokeza unapotokea uchaguzi kunakuwa na kura zisizo halili au kura zilizoharibika wakati Tume imekuwa ikitoa elimu ya mpiga kura katika chaguzi zilizopita.

Bw. Kailima alijibu kuwa kinachosababisha hali hiyo ni ukosefu wa elimu ya mpiga kura kwa wananchi, na ndio maana Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria ya Taifa ya Uchaguzi iliona umuhimu wa kutoa elimu hiyo katika kipindi chote cha mwaka.

“Mkurugenzi tusalie hapo kwenye kura halali na zilizoharibika, elimu hii umekuwa ukiitoa maeneo mbalimbali na leo tuko hapa AFM, kwa nini hadi leo tunakuwa na kura zilizoharibika na kura zisizo halali” alihoji.
 Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani (kulia) akisalimiana na Meneja Mkuu wa Redio AFM ya Dodoma Bw. Tatenda J. Nyawo baada ya kutoa elimu ya mpiga kura kupitia redio hiyo hivi karibuni.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...