Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Uchangiaji wa damu salama unahitajika kutokana na kuwa na wahitaji wengi ambao wanatakiwa kuwekewa katika kuokoa maisha yao.
Hayo ameyasema Afisa Uhamasishaji wa Mpango wa Taifa wa Damu Salama Kanda ya Mashariki , Fatuma Mjungu wakati uchangiaji wa damu katika kiwanda cha Lake Cement kilichopo Kimbiji Manispaa Kigamboni jijini Dar es Salaam , amesema kuwa kwa mwaka jana walikusanya damu chupa 160,000 lakini malengo yake ni ukusanyaji wa chupa 300,000.
Fatuma amesema kutokana na mikakati waliojiwekea kwa mwaka huu watafikia lengo la kukusanya damu chupa 300,000 kwa kuhamasisha wananchi kuchangia damu.

Amesema Lake Cement wamekuwa wakijitoa katika katika suala la uchangiaji damu na kutaka viwanda vingine kujitokeza katika kufanya uchangiaji damu popote pale watawafikia.

Afisa Rasilimali wa Watu wa Lake Cement, Ahmed Nyang’anyi amesema kuwa wanatambua umuhimu wa damu katika kuokoa maisha kwa watu wanaohitaji kwa akina mama wakati wa uzazi na makundi mbalimbali .
Nyang’anyi amesema kuwa wataendelea kuchangia damu kila mwaka kutokana na mahitaji yake kwa wahitaji ni wengi ikilinganishwa na damu iinayokusanywa.

Meneja wa Afya, Mazingira Mahala Pakazi, Happy Mboma amesema hakuna kiwanda kinachozalisha damu hivyo kila mtu anawajibu wa kuchangia damu katika kuokoa maisha wahitaji wa damu.Amesema kuwa wanaochangia damu nao ni wahitaji damu hiyo kwa sababu hakuna mtu ambaye anajua atapata uhitaji damu wakati gani.
Makamu wa Rais wa Kiwanda Lake Cement, Afroz Ansari akizungumza na waandishi wa habari wakati uchangiaji damu katika kiwanda hicho leo jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Kiwanda Lake Cement, Afroz Ansari akiwa katika uchangiaji damu.
Afisa Uhamasishaji wa Mpango wa Taifa wa Damu Salama Kanda ya Mashariki , Fatuma Mjungu akizungumza wakati uchangiaji damu wa kiwanda cha Lake Cement juu ya uhitaji damu katika kuokoa maisha.
Afisa Rasilimali wa Watu wa Lake Cement, Ahmed Nyang’anyi akizungumza wakati wa uchangiaji damu wa kiwanda hicho leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...