Polisi
wanawake kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika
SARPCO,wakimsikiliza Makamu wa Rais,Samia Suluhu Hassan alipokuwa
akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ya siku tatu
Makamu
wa Rais Mh.Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo wakati akifungua
mafunzo ya siku tatu ya polisi wanawake kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya
nchi za kusini mwa Afrika SARPCO,leo katika ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Julius Nyerere,jijini ,Dar es Salaam.Mh Samia ndiye mgeni
rasmi wa mafunzo hayo.Picha na Adam Mzee/VPO.
Makamu
wa Rais Samia Suluhu Hassan akishiriki ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu
ya polisi wanawake kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini mwa
Afrika SARPCO,leo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius
Nyerere,jijini ,Dar es Salaam.Mh Samia ndiye mgeni rasmi wa mafunzo
hayo.Picha na Adam Mzee/VPO.
Makamu
wa Rais Mh.Samia Suluhu Hassan akifuatilia moja ya taarifa wakati wa
ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya polisi wanawake kutoka Jumuiya ya
Maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika SARPCO.Ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Julius Nyerere ,Dar es Salaam.Kushoto kwake ni Mkuu wa
Jeshi la Polisi nchini,IGP Ernest Mangu.
Polisi
wanawake kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika
SARPCO wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mafunzo hayo ya siku
tatu.
Makamu
wa Rais (wa nne kulia) Mh.Samia Suluhu Hassan akishiriki ufunguzi wa
mafunzo ya siku tatu ya polisi wanawake kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya
nchi za kusini mwa Afrika SARPCO,leo katika ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Julius Nyerere,jijini ,Dar es Salaam.Mh Samia ndiye mgeni
rasmi wa mafunzo hayo.Picha na Adam Mzee/VPO
Mafunzo
ya siku tatu ya polisi wanawake kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za
kusini mwa Afrika SARPCO,yakiendele leo katika ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Julius Nyerere,jijini ,Dar es Salaam.Mh Samia ndiye mgeni
rasmi wa mafunzo hayo.Picha na Adam Mzee/VPO.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt.
Augustine Mahiga akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni wakati wa Mafunzo ya siku tatu ya
polisi wanawake kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika
SARPCO,yakiendele leo katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius
Nyerere,jijini ,Dar es Salaam.
Baadhi
ya Askari wanaoshiriki ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya polisi
wanawake kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika
SARPCO,wakiwasili kwa Gwaride katika.Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa
Julius Nyerere ,Dar es Salaam.
Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka
askari polisi wanawake kutoka kwenye Shirikisho la Majeshi la Polisi Kusini mwa
Afrika (SARPCCO) washiriki
kikamilifu katika oparesheni mbalimbali ambazo zinafanyika kwenye ukanda huo kama
hatua ya kukabiliana na vitendo vya uhalifu.
Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli
hiyo wakati akifungua mafunzo ya siku Tatu ya Polisi wanawake kutoka nchi
wanachama wa SARPCCO katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius
Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa
Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewahimiza askari polisi wanawake kufanya kazi
kwa bidii na kujituma hatua ambayo itasaidia kupanda vyeo kama askari wanaume katika maeneo yao ya kazi.Amesisitiza
kuwa muda wa kulalamika kuwa hawapandishwi vyeo umeshapitwa na wakati bali kwa
sasa wachape kazi na waonyeshe kuwa wanaweza majukumu yao wanayopangiwa ili
waweze kupanda vyeo.
“Vyeo haviji tu ni
lazima polisi wanawake muonyeshe kuwa mnaweza ili muweze kupandishwa vyeo na
kupata nafasi za uongozi katika Majeshi yenu”
Kuhusu utendaji
kazi wa Polisi wanawake, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka
polisi hao kutumia mkutano huo wa siku Tatu kujadili kwa kina namna ya kuondoa
changamoto hizo zinazorudisha nyuma utendaji wao wa kazi.
Amesema kama
polisi wanawake wataacha majungu na kujenga umoja na mshikamano miongoni mwao watafikia
malengo yao haraka hasa katika kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya
vitendo vya uhalifu ikiwemo biashara ya dawa za kulevya.
Kwa upande
wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni amesema anaimani kubwa kuwa
mafunzo hayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa polisi hao wanawake kuimarika
ipasavyo katika utendaji wao wa kazi.
Masauni pia
amewahimiza polisi wanawake wanaopata mafunzo hayo kwenda kuwaelimisha na
wenzao mipango na mikakati waliyoweka katika kulinda raia na mali zao katika
nchi zao.BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...