Bw Achiles Bufure, Mkurugenzi Makumbusho 
na Nyumba ya Utamaduni Dar es salaam 

Leo tarehe 18 May ni siku ya Makumbusho Duniani. Kwa hapa Tanzania, Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni itaungana na Makumbusho zote duniani katika kuadhimisha siku hii muhimu. Hivyo watanzania wameshauriwa kuhudhuria kwa wingi katika maadhimisho hayo ili waweze kupanua uwelewa zaidi wa mambo mbali mbali yanayo huyu maisha yao na nchi kwa ujumla. 
Mkurugenzi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar Es Salaam Bwana Achiles Bufure akiongea ofisini kwake ameongeza kuwa katika Maadhimisho hayo, kutakuwa na Onesho maalum litakaloonesha vifaa mbali mbali vya ofisi alivyotumia Muasisi wa Taifa hili Baba wa Taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere, pamoja na mafunzo shirikishi kwa watoto juu ya shughuli za kimakumbusho na Onesho la jukwaani.  
Wananchi mbali mbali wameisifu Mkumbusho na Nyumba ya Utamaduni kwa kuadhimisha siku hiyo kwa kufungua milango hata kwa watu wasio na uwezo wakulipia pindi wanapo tembelea Makumbusho hiyo kwakuwa na wao watapata nafasi adhimu ya kujifunza mambo yanayo husu nchi yao kwa kupitia vioneshwa vilivyopo ndani ya Makumbusho. 
 Maadhimisho hayo ya Siku ya Makumbusho Duniani yatadumu kwa muda wa wiki moja kuanzia leo ili kutoa nafasi kwa watanzania warika mbali mbali kutembelea Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni na kwa tarehe 18 May hakutakuwa na kiingilie cha kuingia na kutembelea maonesho mbalimbali yaliyopo Makumbusho hiyo iliyopo mkabala na chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Dar es Salaam, Posta.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...