Wananchi wa Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa wamejitokeza kwa wingi kusajili Vitambulisho vya Taifa kufuatia maelekezo ya Mkuu wa mkoa huo Mhe. Amina Masenza ambaye amejizatiti kuweka historia ya kuwa mkoa wa kwanza kwa wananchi wake kuwa na Vitambulisho vya Taifa; baada ya kufanikisha kwa asilimia kubwa zoezi la kuwasajili Watumishi wa Umma lililofanyika nchi nzima.

Kwa kuanza; zoezi la Usajili kwa mkoa wa Iringa limeanza katika Wilaya ya Mufindi ambapo zaidi ya wananchi 70,000 wameshajiliwa katika Kata 20 kati ya Kata 36 zilizopo Wilaya humo, huku wananchi 50,000 wakiwa tayari na Vitambulisho vya Taifa.

Akizungumza wakati wa kukagua utekelezaji wa zoezi hilo; Mkuu wa Wilaya ya Mufindi ambako zoezi hilo linaendelea kwa sasa Mhe. Mhe. Jamhuri William amesema “kama Wilaya wamejipanga kuhakikisha zoezi la kuwasajili wananchi linafanyika katika muda mfupi iwezekanavyo na kwamba uhamasishaji umefanyika kwa njia mbali mbali kuhakikisha wananchi wanatumia vema fursa Iliyopo”

Amesisitiza mbali na kuwasajili wananchi; Wilaya ya Mufundi pia inaendelea na zoezi la kuwasajili Wageni na Wakimbizi wanaoishi kihalali Wilayani humo, lengo likiwa ni kupata taarifa sahihi za watu na kuimarisha upatikanaji wa huduma kiurahisi kwa wananchi.

Hivi karibuni Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Amina Masenza alizindua kuanza kwa zoezi la usajili mkoa wa Iringa na kuelekeza kwa kushirikiana na NIDA kila Wilaya kuhakikisha ndani ya siku 60 kuwa wamekamilisha zoezi la kuwasajili wananchi Vitambulisho vya Taifa; na kuwahakikishia wananchi Ofisi yake itahakikisha wananchi wote wakaosajiliwa wanapata Vitambulisho vyao kwa wakati ili matumizi kuanza mara moja.

Wananchi wakipokea maelekezo ya namna ya kushiriki zoezi la Usajili linaloendelea Wilayani Mufindi. 
Baadhi ya wananchi katika Kata ya Ifwagi wakiwa kwenye foleni kusajiliwa zoezi la Vitambulisho vya Taifa linaloendelea Wilayani Mufindi. 
Maafisa wa NIDA wakiendelea na zoezi la uchukuaji alama za Vidole, picha na saini ya Kielektroniki wakati wa zeozi la Usajili likiendelea kwa wananchi wa Wilaya ya Mufindi. 
Afisa Usajili mkoa wa Iringa bwana George Mushi akizungumza jambo na wananchi wa Kata ya Ikongosi wakati wakisubiri kupata huduma ya usajili vitambulisho vya Taifa (NIDA) .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...