Mchezaji nyota wa Mchezo wa Tenisi wa nchini Urusi, Maria Sharapova, amenyimwa kadi maalumu ya kuingia kwenye mashindano ya wazi ya Ufaransa maarufu kama ‘French Open’ yanayotarajiwa kuanza katikati ya Mwezi huu.
Mkuu wa shirikisho wa mchezo wa Tensis nchini Ufaransa, Bernard Giudicelli Ferrandini, alikanusha zaidi ya mara mbili kuwa mchezaji huyo hatoweza kushiriki mashindano hayo na kusema.
“Mwaliko huo ungeliweza kutolewa kwa mchezaji ambaye ametoka kuwa majeruhi lakini sio kwa aliyefungiwa kwa kashfa ya matumizi ya dawa za kusisimua misuli”
“Samahani sana Maria, samahani na kwa mashabiki zake”.
“Pengine nitakuwa nimewaangusha, pengine pia nitakuwa nimemkwaza , lakini ni jukumu langu, wajibu wangu,kuhakikisha ninalinda viwango vya wachezaji katika michezo pasipo shaka yoyote kwamba pengine ametumia madawa ama la kutokana na matokeo.”
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30, na mshindi mara tano wa Grand Slam , aligundulika kutumua madawa yaliyopigwa marufuku michezoni mwaka 2016 katika mashindano ya wazi ya Australia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...