Na Mwandishi Wetu, MOHA.

Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kushirikiana na Benki ya Exim inatarajia kujenga nyumba 9500 za askari magereza ili kukabiliana na changamoto za makazi ya askari  wa jeshi hilo hapanchini.

Akizungumzia changamoto za Makazi ya askari wa Jeshi la  Magereza Nchini, wakati wa uzinduzi wa Gereza la Wanawake wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, alisema Serikali inatambua changamoto za makazi kwa askari magereza na tayari iko katika mazungumzo na benki ya Exim ili iweze kujenga nyumba hizo.

“Nawaomba  askari wetu nchi nzima  wawe na subira  Serikali inatambua na  inashughulikia changamoto ya makazi ya  askari na tayari tuko katika mazungumzo na wadau ikiwemo benki ya Exim kuanza mradi wa ujenzi wa nyumba takribani 9500, lengo ni kukidhi kiu ya makazi ya askari na familia zao,” alisema Masauni.

Awali akitoa maelezo ya ujenzi wa Gereza hilo, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, Dk. Juma Malewa alisema ujenzi wa Gereza hilo umefanywa na wataalamu ambao ni askari Magereza kwa  kushirikiana na wafungwa kama sehemu ya utekelezaji wa  amri ya Mh. Rais Dk. John Magufuli ya kutaka wafungwa watumike katika kazi za uzalishaji ikiwemo kilimo,ujenzi na ufundi mbalimbali.

Ujenzi wa Gereza hilo umegharimu jumla ya shilingi milioni 65 na litasaidia pia  kuhifadhi wafungwa 148 na hivyo kupunguza msongamano wa wafungwa katika Gereza la Kongwa mkoani Dodoma pamoja na kuepuka usumbufu wa  ndugu wa wafungwa kusafiri mpaka wilayani Kongwa kwenda kuwaona ndugu zao.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akishirikiana na Viongozi wengine kufungua Gereza  la Wanawake wilayani Mpwapwa  lililojengwa na wataalamu ambao ni askari magereza kwa  kushirikiana na wafungwa.Ufunguzi huo umefanyika wilaya ya Mpwapwa, mkoani Dodoma.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Gereza la Wanawake wilayani Mpwapwa  lililojengwa na wataalamu ambao ni askari magereza kwa kushirikiana na wafungwa.Gereza hilo limegharimu jumla ya shilingi milioni 65 .Ufunguzi huo umefanyika wilaya ya  Mpwapwa, mkoani Dodoma.
 Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa, Mheshimiwa George Lubeleje , akizungumza wakati wa ufunguzi wa Gereza la Wanawake wilayani Mpwapwa  lililojengwa na wataalamu ambao ni askari magereza kwa kushirikiana na wafungwa.Gereza hilo limegharimu jumla ya shilingi milioni 65 .Ufunguzi huo umefanyika wilaya ya Mpwapwa,mkoani Dodoma.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, Dk. Juma Malewa,  akizungumza wakati wa ufunguzi wa Gereza la Wanawake wilayani Mpwapwa  lililojengwa na wataalamu ambao ni askari magereza kwa kushirikiana na wafungwa.Gereza hilo limegharimu jumla ya shilingi milioni 65 .Ufunguzi huo umefanyika wilaya ya  Mpwapwa,Mkoani Dodoma.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wa pili kulia), akiongozana na Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Dk. Juma Malewa (kulia) kuelekea katika eneo lilipo  Gereza la Wanawake Mpwapwa, lililojengwa na wataalamu ambao ni askari magereza kwa kushirikiana  na wafungwa.Gereza hilo limegharimu jumla ya shilingi milioni 65 .Ufunguzi huo umefanyika wilaya ya  Mpwapwa,mkoani Dodoma.

Wananchi wa Mpwapwa wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa Gereza la Wanawake wilayani Mpwapwa lililojengwa na wataalamu ambao ni  askari magereza kwa kushirikiana  na wafungwa.Gereza hilo limegharimu jumla ya shilingi milioni 65 .Ufunguzi huo umefanyika wilaya ya  Mpwapwa,mkoani Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...