Havas Group ni moja kati ya mawakala wakubwa wa matangazo ya biashara yenye mtandao mpana duniani kote. Ikiwa na makao makuu nchini Ufaransa, Havas inapatikana katika nchi 149 zikiwemo nchi 19 barani Afrika ambapo wana ubia na kampuni nyingine. Havas Group,imegawanyika mara mbili katika Afrika - Havas Media Africa & Arena Media Afrika.
Kihistoria, Havas imejikita kwa nguvu zaidi kwenye nchi zinazoongea lugha ya kifaransa zikiwemo,Cameroon, DRC, Ivory Coast & Senegal kuwa ndio nguzo yao katika ukanda huo. Nyingine ni pamoja na Gabon, Niger, Burkina, Benin, Togo. 
Hivi karibuni,Havas imekuwa kwa kasi katika ukanda wa Afrika Mashariki, ikianzia na Kenya kwa miaka 5 iliyopita. Uganda na Rwanda zilifunguliwa mwaka jana wakati Zambia ipo kwenye  mipango ya kufunguliwa mwishoni mwa mwaka  huu. Ofisi za Tanzania zimekuwa zikifanya kazi tangu mwaka 2015 na tangu wakati huo hakuna kurudi nyuma. Hadi sasa tayari ina wateja wa kimataifa kama vile Emirates, Airtel & DTCM, biashara ya Tanzania inakua kulingana na mahitaji ya soko la media linaloongezeka siku hadi siku. 
Shughuli za Havas Africa huratibiwa na kusimamiwa na kitengo cha Havas Afrika chenye makao makuu mjini Paris,ikikuza utaalamu kimataifa, zana na maarifa kwa masoko yote.Mtindo wao wa kufanya kazi huhakikisha kwamba kuna uthabiti na utendaji bora  katika matawi yao yote, ili kuinua na kuleta mawakala wote kwenye kiwango cha ubora kilicho sawa. 
Kinachoitofautisha Havas  ni mbinu za utumiaji wa takwimu na namna yao ya kipekee ya kuweka matangazo ya bidhaa kwenye mtandao. Ndani ya mazingira ya Afrika, Havas  tayari imepiga hatua mbele na kuona umuhimu wa  vitu hivi viwili  katika kufanya mapendekezo na maamuzi. 
Meneja uendeshaji wa Havas Tanzania anasema mwaka jana umekuwa ni mwaka wa kusisimua sana katika suala la maendeleo ya ofisi yake na timu kwa ujumla inaona fursa kubwa mwaka 2017. Mbinu kubwa wanayoitumia kwa mteja wao,ni kuwa na uelewa wa soko la Tanzania, mteja wake anataka nini na namna pekee wanayotumia kutangaza bidhaa kupitia mtandao, na namna wanavyoweza kujenga fikra  kimkakati kwa kuongozwa na  takwimu.
Hii ndiyo sababu inayowafanya wateja wengi kuchagua Havas.
 Kwa mawasiliano na Havas Tanzania: fey.mallonga@tanzania.havasafrica.com


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...