Na Karama Kenyunko- blogu ya jamii.

Mkulima mmoja Samwel Nicodem Bwandu 38, amehukumiwa kwenda jela miaka 20 baada kupatikana na hatia ya kukutwa na vipande nane vya meno ya tembo vyenye thamani ya milioni 60.

Hukumu hiyo imesomwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shahidi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Akisoma Hukumu, huyo hakimu shahidi amesema kuwa, upande wa mashtaka umeweza kuthibitisha mashtaka bila ya kuacha shaka kuwa kweli Bwandu alikutwa na meno ya tembo lakini haukuweza kuthibitisha kuwa alikuwa akijihusisha na biashara hiyo.

Hata hivyo, mahakama hiyo,imemuachia huru Kidamisi Kidarageda Kidiwami, Mkazi wa Iringa baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yake kuwa alihusika katika tuhuma hizo za meno ya tembo.

Watuhumiwa wote wawili, Bwandu na Kidawami walikuwa wakituhumiwa kwa makosa ya kupatikana na nyara za serikali ambazo ni vipande nane vya meno ya tembo vyenye thamank ya milioni 600 na Kijihusisha na nyara hizo zenye thamani ya milioni 900.

Hakimu Shahidi amesema, amezingatia ushahidi wote uliotolewa na upande wa mashtaka na utetezi wa washtakiwa na kuridhika kwamba mshtakiwa Kidawami hakuhusika katika kutenda makosa hayo.

"Hakuna shahidi yeyote aliyefika mahakamani hapo na kuthibitisha kuwa mshtakiwa wa Kidawami alihusika na tuhuma hizo, isipokuwa shahidi namba tano ambaye nae alikuwa na ushahidi wa kusikia tu", amesema hakimu Shahidi"

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...