Na  Bashir  Yakub.

Ndio  ni  kweli  mwanamke  aliyeolewa  anaweza  kukopa  hela  kwa  jina  la  mme  wake.  Tena  kukopa  kwenyewe   si  lazima  awe  amepata  ridhaa  au  ruhusa   kutoka  kwa  mme  wake.   

Pia  si ruhusa  tu  bali  si  lazima   amtaarifu  mme  huyo. Sheria  ya  ndoa  , sura  ya 20 iliyofanyiwa  marekebisho  mwaka  2010  ndiyo iliyoeleza  jambo  hili . Lipo kifungu  cha  64  cha  sheria  hiyo.

Kwa  ujumla  makala   haya  yatatizama  jambo  hili  likoje,  linahusisha nini  na  nini, vigezo   na  sifa  za  kufanya  hivyo na  mambo  mengine  ambayo  yanalizunguka  jambo  hili  lakini  kwa  ufupi.

1.MWANAMKE  GANI  ANAWEZA  KUKOPA.

Kifungu  hicho  kimesema mwanamke  anayeweza  kukopa  ni  yule   aliye  kwenye  ndoa  inayotambulika  kisheria.  Ikiwa  mwanamke  hayupo katika  ndoa  ambayo  sheria inaitambua  basi  haki  hii  ya  kukopa  kwa  jina  la  mme  wake  anaikosa. 

Ikiwa  mmetengana  lakini  ndoa  haijavunjika  kisheria  basi  haki  hii inaendelea  kubaki.  Isipokuwa  tu  itaondoka  ikiwa  mmetengana  kwa  makubaliano  maalum  ambapo  matunzo  na  matumizi  yote  mwanamke  anapata  bila  wasiwasi.

Pia  ikiwa  kuna  talaka  basi  mwanamke  hawezi  kukopa  kwa  jina  la  mme  wake  kwa  kuwa  talaka  kisheria   inavunja  ndoa  na  hivyo  tafsiri yake  ni  kuwa  hakuna  ndoa.  Lakini  kukiwa  na  shauri  la  talaka  mahakamani  na  ndoa  haijavunjwa  rasmi  na  mahakama  basi  haki  hii  inaendelea  kubaki  kwa  mwanamke  huyo.

2. KWANINI  SHERIA  IMEMRUHUSU  MWANAMKE  KUKOPA  KWA  JINA  LA  MME  .

Sheria  imemruhusu  mwanamke  kukopa  kwa  jina  la mme  wake  tena  bila  hata  ridhaa  ya  mme  wake  kwakuwa   imempa  wajibu  mume  kumtunza  mke  wake  na  mtoto/watoto  kama  yupo.  Kwa  mujibu  wa  sheria  ya  ndoa  ni  lazima  mume  kumtunza  mke  wake  pamoja  na watoto  kama  wapo. 

Kwa  upande  mwingine  mwanamke  naye  anaruhusiwa  kumtunza  mme  wake  lakini  kwake  sio  lazima.  Sheria  haijampa  ulazima  mwanamke  bali  mwanaume .  Kwahiyo  ni  katika  mazingira  haya  ambapo   suala la  mke  kukopa    bila  ridhaa  ya  mme  wake   tena  kwa   jina  la  mme  huyo  linapokuja. 

Hata  hivyo  sio  wakati  wote  mwanamke  anaruhusiwa  kukopa  kwa  njia  hiyo  bali  ni pale  tu  mume  wake  anapokaidi  wajibu  wake  wa  lazima  wa  kumpa  matunzo/matumizi.  Hapa  ndipo  mwanamke  anaweza  kukopa    kwa  jina  la  mme  wake  tena bila  hata ridhaa  ya  mme  huyo.

 Mke  hataruhusiwa  tu   kufanya  hivyo  kwa  kutopewa  mahitaji  yake  pekee  bali pia  hata  kama  ana watoto/mtoto   nao  hawajapewa  mahitaji  basi  hata  hapo  anaruhusiwa  kukopa. 



                      KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...