Wauguzi wilayani Kishapu wamepongezwa kwa kazi nzuri na
kutakiwa kuendelea kuipenda kazi yao kuchapa kazi katika mazingira yoyote
waliopo kwani wao ni chachu ya afya katika jamii.
Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani
Shinyanga, Nyabaganga Talaba wakati kwenye kilele cha Siku ya Wauguzi Duniani
iliyofanyika katika viwanja vya Hospitali ya Wilaya ya DK. Jakaya Kikwete.
Talaba ambaye aliwaongoza wauguzi hao na watumishi wa
halmashauri kutoa misaada na kufariji wagonjwa hospitalini hapo aliwapongeza
kwa huduma nzuri kwa wagonjwa.
Alisema kuwa bila ya wauguzi afya haijakamilika na kuwa
uuguzi ni zaidi ya wito na ni huduma inayohitaji upendo na huruma kwa wale
unaowahudumia.
“Kama huna upendo na ukarimu basi wewe siyo muuguzi na
ukionesha ukarimu na upendo ndiyo mwanzo wa kupona kwa mgonjwa ukifika tu pale
mgonjwa anapona hata kabla hujampa dawa,” alisisitiza.Aidha, aliwataka wauguzi waendelee kuwa na ushirikiano
baina yao huku akiwapongeza kwa mafanikio katika sekta ya afya pamoja na kuwa
wana changamoto ya mazingira ya kazi.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Talaba akiwa amembeba mtoto aliyezaliwa katika Hopsitali ya Wilaya (Dk. Jakaya Kikwete) wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani kiwilaya.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Nyabaganga Talaba akimpa msaada mmoja wa mama anayeuguza mtoto katika hopsitali ya wilaya.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Talaba akizungumza na wauguzi (hawapo pichani) katika sikukuu ya Wauguzi Duniani viwanja vya hospitali ya wilaya.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...