Mradi wa “Hakuna Wasichoweza” unaoendeshwa kupitia taasisi ya
Vodacom Tanzania Foundation na kutekelezwa kwa ushirikiano wa Shirika
lisilo la Kiserikali la T-Marc katika mkoa wa Lindi unazidi kuleta faraja kwa
watoto wa kike ambapo kwa mwaka huu wasichana wapato 2,000 tayari
wamenufaika nao.
Mradi huu ni mwendelezo wa program ya Hakuna
Wasichoweza uliozinduliwa miaka ya nyuma-Mtwara, umewafikia
wanafunzi na walimu 10,000 mashuleni kupatiwa elimu ya afya ya uzazi na
huduma ya vifaa vya kujisitiri (pedi) wakati hedhi kwa watoto wa kike.
Akiongea na mtandao huu Meneja ruzuku na Mawasiliano wa Vodacom
Tanzania Foundation,Sandra Oswald alisema tangu mradi huu uanze
umekuwa na mafanikio makubwa kwa kufikia idadi kubwa ya walengwa
wanaosoma katika shule mbalimbali mkoani Lindi ambapo wameweza
kupatiwa elimu kuhusiana na mabadiliko ya miili yao katika mchakato wa
makuzi na wamewezeshwa kwa kupatiwa taulo za hedhi, Alisema Oswald.
Naye mmoja wa wanafunzi walionufaika na mradi huu, Riziki Athuman (14)
ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi ya
Tandangongoro akiongea kwa niaba ya wenzake kuwa “Hivi sasa
wanaelewa kuhusina na suala zima la hedhi na jinsi ya kukabiliana nalo
hususani kujiweka katika hali ya usafi na kutumia taulo za kisasa ambazo
zinatuwezesha kuendelea na masomo tofauti na awali ambapo wasichana
wenzangu wengi walishindwa kuhudhuria vipindi shuleni wanapokuwa
kwenye hedhi kutokana na kutokuwepo na mazingira rafiki.
Suala la hedhi
lilikuwa halizungumziwi kabisa tofauti na sasa ambapo linajadiliwa na
kutafutiwa suluhisho la kukabiliana na changamoto zake hususan kujenga
vyoo na miundombinu ya maji mashuleni ya kuwasaidia watoto wa kike
wanapokuwa kwenye hedhi”. Alisema Riziki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...