Serikali
kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) imekusanya shilingi
bilioni 63,015,450,230 kwa kipindi cha Octoba 2013 mpaka Februari 2017
tangu kuanzishwa kwa mtambo wa kuhakiki na kusimamia Huduma za
Mawasiliano(TTMS) nchini.
Hayo
yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Edwin
Ngonyani wakati akijibu swali la Mbunge wa Kigamboni.
“Mtambo
huu umesaidia Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) kuongeza ufanisi
katika kusimamia Sekta ya Mawasiliano pamoja na kwenda sambamba na kasi
ya mabadiliko yanayotokea katika Sekta ya Mawasiliano Duniani
kote,”aliongeza Ngonyani
“Kuanzia
Oktoba 2013 hadi Februari 2017, kiasi cha shilingi 63,015,450,230
zilipatika na katika hizo bilioni 56,987,368,631 zimewasilishwa hazina
na shilingi bilioni 6,028,081,599 zimewasilishwa Tume ya Sayansi na
Teknolojia(COSTECH) kwa ajili ya kugharamia tafiti mbalimbali zenye
manufaa kwa nchi yetu ambapo kabla ya mfumo huu mapato hayo hayakuwepo.”
“Aidha
pamoja na mafanikio hayo jitihada za kuboresha zaidi mfumo huu ili
kuweza kubaini na kujiridhisha juu ya mapato yote yatokanayo na huduma
za mawasiliano na yanayokidhi mahitaji ya Mamlaka ya Mapato
Tanzania,Benki kuu ya Tanzania na TCRA zinaendelea,” aliongeza Naibu
waziri Ngonyani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...