Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mheshimiwa Kisare Makori amekabidhiwa Mwenge wa Uhuru na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Ally Happi tayari kwa kuzuru katika Miradi mitano ya Maendeleo katika Manispaa ya Ubungo.

Akizungumza wakati wa Makabidhiano hayo Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori amesema kuwa Mwenge wa Uhuru umezuru kwa Mara ya Kwanza katika Wilaya mpya ya Ubungo hivyo historia mpya imeandikwa.

Alisema kuwa Mwenge wa Uhuru Kwa Mwaka 2017 katika Wilaya ya Ubungo utakimbizwa umbali wa Kilomita 46 na gharama ya Miradi yote Mwenge utakapopita ni Zaidi ya Bilioni 2.8

Mwenge wa Uhuru Mwenye kauli mbiu ya kutilia msisitizo kushiriki Kukuza Uchumi wa Viwanda kwa Maendeleo ya Nchi yetu umebeba jumbe mbalimbali ikiwemo ile ya Mapambano dhidi ya dawa za kulevya, tuwajali na tuwasikilize watoto na vijana utakapomaliza kutembelea Miradi ya Maendeleo katika Wilaya ya Ubungo utaelekea Mkoani Pwani.

Katika mbio za Mwenge Umebaba ujumbe mwingine wa kuhamasisha kupungua kwa maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, Unyanyapaa na vifo vitokanavyo na UKIMWI.

Aidha watanzania wameombwa kushiriki kutokomeza Malaria kwa Manufaa ya Watanzia na jamii kwa ujumla.

Imetolewa Na;
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...