Profesa Honest Prosper Ngowi akiwaelekeza baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe kuhusu utafiti unaoangazia masuala ya kodi. Kulia ni Profesa Arne Wiig akitoa maelekezo kwa mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho. Utafiti huo unafanywa kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Christian Michelsen Institute (CMI) ya Norway na Chuo Kikuu Mzumbe cha nchini Tanzania.

Wanafunzi wa Mzumbe Dar Es Salaam wakifanya shughuli za utafiti kwa vitendo katika mradi wa utafiti wa mambo ya kodi. Mradi huu ni ushirikiano kati ya taasisi ya Christian Michelsen Institute (CMI) ya Norway na Chuo Kikuu Mzumbe. 

Unafadhiliwa na Baraza la Utafiti la serikali ya Norway na upo katika mwaka wa mwisho katika miaka yake mitatu. Professor Ngowi wa Mzumbe ni mtafiti mkuu katika mradi huu Tanzania. Watafiti kutoka Norway waliokuwepo Mzumbe ni Prof. Odd Fjeldstad na Prof. Arne Wiig. 

Katika utafiti huu wanafunzi walijibu maswali mbalimbali yahusuyo kodi. Matokeo yake yatatumika kushauri mamlaka kuhusu mambo kadhaa ya kodi Tanzania. Utafiti wa aina hii unafanyika pia Angola na Zambia.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe wakiendelea na utafiti huo jijini Dar es Salaam jana.
Wanafunzi wengine wakijadiliana jambo katika Chuo Kikuu cha Mzumbe ambako utafiti huo unaendelea leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...