SHIRIKA
la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limetoa semina juu ya umuhimu wa
hifadhi ya jamii kwa wanacama wa kikundi cha Umoja wa Miradi ya Viziwi
Tanzania UMIVITA.
Semina hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na shirika hilo ambapo ilihusisha wanachama wapatao mia mbili.
Akizungumza katika semina hiyo Ofisa Matekelezo Mkuu wa NSSF Mkoa wa Temeke, Nuhu Ramadhani alisema wanachama hao walipata fursa ya kuifahamuvizuri NSSF na kujua mafao yanayotolewa na shirika hilo yakiwemo pensheni ya uzeeni,pensheni ya ulemavu,pensheni ya urithi, msaada wa mazishi, mafao ya kuumia kazini, mafao ya uzazi na matibabu bure kwa mwananchama na wategemezi wake.
Aisha NSSF ilitoa fursa kwa Wanachama wa UMIVITA waliohudhuria semia hiyo kujiandikisha kuwa wanachama.
Ofisa Uhusiano na Masoko wa NSSF, Anna Nguzo, akizungumza wakati wa semina iliyoandaliwa na NSSF wa ajili ya wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania.
Ofisa Matekelezo Mwandamizi wa NSSF Mkoa wa Temeke, Naphisa Jahazi, akizungumza wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Miradi kwa Viziwi (UMIVITA), Jamal Amiri akizungumza wakati wa semina iliyoandaliwa na NSSF kwa ajili ya wanachama wa Kikundi cha Umoja wa Miradi kwa Viziwi Tanzania.
Wanasemina.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...