Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa akizungumza wakati wa kikao cha pamoja baina ya wataalam kutoka Kampuni ya esri- inayojishughulisha na kutoa huduma za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS), walipokutana leo Jijini Dar es Salaam ili kujadili namna mfumo huo unavyoweza kutumika wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu mbalimbali nchini. Kulia ni Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Shirila la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA Tanzania) Dkt. Hashina Begum.
Mtalaam kutoka kampuni ya esri – inayojishughulisha na kutoa huduma za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS), Bi. Linda Peters akielezea jambo wakati wa kikao baina ya wataalam kutoka Kampuni hiyo na Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni wataalam kutoka Kampuni hiyo Bw. Patrick Kipchumba na Mhandisi Anthony Gakobo.
Baadhi ya wataalam kutoka Kampuni ya esri – inayojishughulisha na kutoa huduma za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS), wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) walipokutana leo Jijini Dar es Salaam ili kujadili namna mfumo huo unavyoweza kutumika wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu mbalimbali nchini.
Mtalaam wa Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS) Anthony Gakobo akionyesha moja ya kifaa kinachotumika katika kuhakiki uhalisia wa taarifa za kijiografia mbele ya Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni watalaam wa mfumo huo Bw. Patrick Kipchumba na Bi. Linda Peters.
Mshauri wa Masuala ya Kitakwimu kutoka Benki ya Dunia – Tanzania, Bi. Elizabeth Talbert akifafanua jambo wakati wa kikao cha pamoja baina ya wataalam kutoka Kampuni ya esri- inayojishughulisha na kutoa huduma za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS) na menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ili kujadili namna mfumo huo unavyoweza kutumika wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu mbalimbali nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi kutoka UNFPA, Benki ya Dunia – Tanzani , watalaam kutoka Kampuni ya esri inayojishugulisha na kutoa huduma za Mfumo ya Taarifa za Kijiografia (GIS) pamoja na Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) mara baada ya kumaliza kikao kujadili namna mfumo wa GIS unavyoweza kutumika wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu mbalimbali nchini.

(Picha zote na Frank Shija – MAELEZO) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...