Unapomuongelea MAKEKE si jina geni kwenye Tasnia ya mitindo nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla. Mwaka jana alikuja na collection ya aina yake iliyoitwa TABID - The African Beauty in The darkness, ( uzuri wa Afrika gizani) collection hio imefanya vizuri sana 2016/2017 kwani imeoneshwa kwenye Majukwaa mbalimbali makubwa ya mitindo. Na mwaka huu mwanamitindo huyu asiyeishiwa MAKEKE amekuja na kitu kipya kabisa, kinachoitwa OTOSIM2017 - ON THE OTHER SIDE OF MAKEKE, akiwa na maana ya ladha/ubunifu wa aina Nyingine. Kwa Mara ya kwanza OTOSIM imeoneshwa kwenye jukwaa kubwa la ZANZIBAR SWAHILI FESTIVAL mwezi uliopita na kufanya maajabu makubwa jukwaani. Kwa watu waliokuwepo pale walijionea utamu wa show hiyo ya Ki - MAKEKE. Msanii huyu wa mitindo ameahidi mambo mengi matamu zaidi kwa mwaka huu 2017. Tuendelee kusubiri.
Home
Unlabelled
OTOSIM 2017 BY MAKEKE NI MOTO WA KUOTEA MBALI!
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...