Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
(wa pili kushoto) alipokuwa akiangalia jengo la ZSTC Mkoani Pemba
lililoanguka ukuta kutokana na kuangukiwa na mti baada ya mvua kubwa za
masika zilizonyesha hivi karibuni na kusababisha uharibifu mkubwa
alipofanya ziara maalum leo (kushoto) Waziri wa Biashara Viwanda na
Masoko Mhe, Amina Salum Ali.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
(kushoto) alipofika kijiji cha Gando kumfariji na kumpa pole Mzee Juma
Mjaka Khamis (kulia) akiwa na Familia yake aliyepata maafa ya nyumba
yake kuangukiwa na mti na kupelekea kukosa sehemu ya kuishi baada ya
mvua kubwa za masika zilizonyesha hivi karibuni kisiwani humo.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
(kushoto) alipokuwa akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkoani
Mkoa wa Kusini Pemba Mhe,Hemed Suleiman alitembelea Kijiji cha Makombeni
Wilaya hiyo kuangalia nyumba mbali mbali za Wananchi zilizopatwa na
athari zilizotokana na Mvua zinazoendelea kunyesha kisiwani humo leo
wakati alipofanya ziara maalum ya kikazi.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
(katikati) alipofika katika daraja la Chamanangwe leo kisiwani Pemba
lililokatika kutokana na maji ya Mvua zilizonyesha hivi karibuni na
kusababisha usumbufu kwa wanaotumia daraja hilo kutoka upande mmoja
kuelekea sehemu nyengine wakati alipofanya ziara maalum ya siku moja
ya kikazi (Picha na Ikulu).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...