Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo 

WAKULIMA wa matunda wametakiwa kulima kwa kutumia mbegu bora na kilimo cha kisasa ili kupata soko kwenye viwanda vinavyosindika zao hilo, ndani na nje ya nchi. Aidha wananchi wameshauriwa kulima kilimo kinachostahimili ukame ikiwemo mahindi, mihogo, viazi vitamu na mikunde ili kujihadhali na baa la njaa baadae

Hata hivyo wametakiwa kuhifadhi chakula wakati wa mavuno utakapofika kwani kwa kufanya hivyo itawasaidia kuwa na akiba ya kutosha. Rai hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo, alipotembelea kiwanda cha Elven Agri company ltd kilichopo Mapinga na kiwanda cha Sayona kinachomilikiwa na kampuni MAMA ya MMI steel, kilichopo kata ya Mboga wilayani Bagamoyo.

Alieleza, wakulima wengi wanahitaji kulima kwa tija badala ya kupata hasara kwa kukosa masoko. Mhandisi Ndikilo alisema, kwa kutambua hilo, kuna kila sababu ya kubadilika kwa kuona umuhimu wa kulima matunda yaliyo na rutuba bora na yanayojiuza. 

"Wataalamu wa kilimo, watendaji wa halmashauri katika idara hii, mtoke maofisini muende kuwapa elimu wakulima hawa ili waweze kujifunza kulima kwa kutumia mbegu za msimu mfupi, kuweka pembejeo na kupalilia, Kwa kutoa elimu za mara kwa mara kwa kufuata teknolojia za kisasa, lazima waende na wakati ili waweze kunufaika kwa jasho lao "alisema mhandisi Ndikilo. 
Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo, aliyeshika ndizi, akionyeshwa hatua za uzalishaji katika usindikaji wa matunda kwenye kiwanda cha kusindika matunda cha Elven Agri co. Ltd kilichopo Mapinga, Bagamoyo.
Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto) akionyeshwa namna bidhaa mbalimbali kama pilipili zinavyofungashwa katika kiwanda cha kusindika matunda cha Elven Agri co. Ltd kilichopo Mapinga Bagamoyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...