Na Asteria Muhozya, Arusha
Wadau wa Madini nchini wametakiwa kujikita katika shughuli za ukataji na usanifu wa madini badala ya kusanifiwa nje ya nchi ili kuwezesha  adhma ya Serikali ya Tanzania ya Viwanda kupitia  Sekta ya Madini.
Hayo yalisemwa na Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi  Benjamini Mchwampaka wakati wa kufunga Maonesho ya 6 ya Kimataifa ya Madini ya Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 3-5 Mei,2017.
Aliongeza kuwa, uwepo wa shughuli za ukataji na unga'rishaji wa madini hayo nchini kutawezesha kuyaongezea thamani ikiwemo kupanua wigo wa ajira kupitia sekta ya madini.
" Tanzania ya sasa ni ya Viwanda. Na sisi sekta ya madini tuwe na viwanda vyetu  vya kusanifu madini yetu hapa hapa nchini. Kwanza tutayaongezea thamani madini yetu lakini pia tutazalisha ajira kwa wingi," alisema Mchampaka.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo (katikati), Waziri wa Madini na Maendeleo ya Viwanda wa Nigeria  Abubakar Bwari (wa pili kulia), Katibu  Mkuu wa Wizara ya Madini na Maendeleo ya Viwanda wa Nigeria,  Abbas Mohamed (wa kwanza kulia) , Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Arusha Peter Pereira ( wa kwanza kushoto ) na Mwenyekiti wa Chama Cha Wafanyabiashara wa Madini Tanzania Sam Mollel (wa pili kushoto) wakifuatilia kutangazwa kwa washindi wa Mnada wa Madini ya Tanzanite.
 Kamishna wa Madini Tanzania Mhandisi Benjamin Mchwampaka (katikati) akikata kamba maalum katika masunduku  yaliyowekwa  bahasha za walioomba kununua madini ya Tanzanite kupitia mnada. Kulia ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Shirika la Madini la Taifa, (STAMICO) Mhandisi Hamis Komba na kushoto ni Mwakilishi kutoka Kampuni ya TanzaniteOne, Husein Gonga. 
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo (kulia) akiangalia zawadi kabla ya kumkabidhi Waziri wa Madini na Maendeleo ya Viwanda wa Nigeria, Mhe. Abubakar Bwari (kushoto).

 Baadhi wa washiriki wa  Maonesho ya 6 ya Madini ya Vito Arusha wakiwemo wanunuzi na wauzaji wakifuatilia hatua za kumpata mshindi wa Mnada wa Madini ya Tanzanite.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya SDK Limited, Bi. Susie Kennedy akimwonesha Waziri wa Madini na Maendeleo ya Viwanda wa Nigeria,  Mhe. Abubakar Bwari bidhaa za madini zinazotengenezwa na kampuni hiyo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...