Baadhi ya wauguzi na madaktari wakimpandisha kwenye ambulance Mtoto Antonia kwa ajili ya kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), imemsafirisha mtoto, Antonia Justine Msoka anayeongezeka uzito kwenda India kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.

Mtoto Antonia mwenye umri wa miaka 17 alikuwa amelazwa Muhimbili tangu Novemba mwaka jana na kuanza kupatiwa matibabu.

Akizungumzia afya yake, Antonia amesema kuwa afya yake inaendelea vizuri na amewashukuru madaktari na wauguzi wa Muhimbili kwa kumpatia matibabu.

“Nashukuru kwa msaada kwani sasa naenda Hospitali ya India kwa matibabu zaidi, naishukuru pia serikali kwa kunisadia,” amesema mtoto Antonia.

Awali Antonia alifikishwa Muhimbili akiwa na uzito wa Kilo 250, lakini sasa zimepungua na kufikia kilo 230.

Mama wa mtoto huyo, Salome Manyirizu Kisusi ameishukuru wizara hiyo kwa msaada fedha za matibabu na kumsafirisha kwenda India kwa ajili ya matibabu zaidi.

“Nawashukuru watu waliokuwa wakiniombea na pia wote walionichangia fedha za matumizi, Mungu awabariki. Pia, nawashukuru madaktari, wauguzi na uongozi wa Muhimbili kwa ushirikiano mzuri walionipatia,” amesema Mama Salome.
Mtoto Antonia akiwa amepumzika kwenye gari ya kubebea wagonjwa leo kabla ya kupanda ndege kuelekea India.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...