Taasisi na Asasi Zisizokuwa za Kiserikali za Tanzania (NGOs) taasisi za serikali zinazoshughulikia uwajibikaji na wadau wengine kadhaa walikutana hivi leo  ili kufanya tathmini ya hatua zilizopigwa na mafunzo yaliyopatikana wakati wa uhai wa mradi wa Pamoja Twajenga  unaofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID). Toka mwaka 2013, watendaji wa mradi wa Pamoja Twajenga wamekuwa wakifanya kazi bega kwa bega na asasi za kiraia na taasisi za serikali ya Tanzania zinazoshughulikia masuala ya uwajibikaji ili kuimarisha mahusiano kati ya asasi za kiraia na serikali. Mradi huu ulitoa mafunzo na msaada kwa jumla ya asasi zisizo za Kiserikali 16 na taasisi tatu za serikali zinazojihusisha na uwajibikaji katika mikoa ya Mtwara, Iringa, Dodoma, Morogoro na  Zanzibar kwa lengo la kukuza uwazi na uwajibikaji wa serikali kwa raia wa Tanzania. 
Kutokana na msaada huu, hivi sasa asasi za kiraia na taasisi za uwajibikaji zilizoshiriki zina uwezo zaidi wa kushiriki katika mijadala kuhusu masuala mahsusi yanayozigusa jamii (issue-based dialogue).
Raia katika mikoa lengwa ya mradi – ikiwa ni ni pamoja na vijana, wanawake na makundi mengine ya watu wanaowekwa pembezoni wana uwezo zaidi wa kujadiliana na serikali zao kuhusu kero zao, jambo ambalo limeongeza uwajibikaji na uwazi katika usimamizi wa rasilimali za umma na katika ufanyaji maamuzi
. Asasi za kiraia zilizosaidiwa na mradi wa Pamoja Twajenga zinafanya kazi katika masuala yanayohusiana moja kwa moja na mahitaji ya msingi ya raia ikiwa ni pamoja na huduma za afya, elimu, usalama wa chakula na usimamizi wa rasilimali. 
 Majadiliano ya jumuiya katika kata ya Mpapula mkoani Mtwara, mwanajamii akielezea uzoefu wao kuhusu vitendo vya ukatili vinavyofanywa dhidi ya wanawake na watoto. Majadiliano hayo yaliandaliwa na asasi ya kiraia ya Wanasheria Wanawake Katika Maendeleo Afrika (Women in Law and Development in Africa - WiLDAF), mojawapo kati ya asasi za kiraia zilizopokea msaada kutoka mradi wa Pamoja Twajenga uliokuwa ukifadhiliwa na USAID. (Picha kwa hisani ya: Rhoda Nashon/WiLDAF)
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...