NA K-VIS BLOG/Khalfan Said.
SHIRIKA
la Umeme Tanzania, (TANESCO), limewaomba wateja wake na wananchi kwa
ujumla kutoa taarifa mapema mara inapotokea hitilafu ya umeme
iliyosababishwa na mvua au sababu nyingine.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Mei 11,
2017, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka, (pichani
juu), alisema, sambamba na hilo pia wananchi wasifanye shughuli au kukaa
chini ya miundombinu ya umeme.
“Lakini
tunawaomba wananchi watoe taarifa haraka maeneo yenye mafuriko au
mkusasnyiko wa maji mengi ili wataalamu wetu waweze kuchukua hatua za
haraka.” Alisema.
Dkt.
Mwinuka pia alisema endapo kuna nyaya, nguzo au kifaa chochote cha
umeme kimepata hitilafu na kinahatarisha maisha ni vema uangalizi au
alama ikawekwa ili kuwapa hadhari wapiti njia na watoto wasikaribie eneo
hilo wakati mafundi wa TANESCO wakichukua hatua za marekebisho.
Mamlaka
ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA), katika taarifa yake iliyotoa Mei
9, 2017 imeonya kuwa maeneo ya Pwani ya Kaskazini ikiwemo visiwa vya
Unguja na Pemba, yatakabiliwa na vipindi vifupi vya mvua kubwa inayozidi
milimita 50 ndani ya saa 24 kuanzia Mei 10 hadi 12, 2017.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Dkt. Tito
Mwinuka, (katikati), akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake
jijini Dar es Salaam, Me11, 2017. Dkt. Mwinuka ametoa hadhari kwa
wananchi kutogusan miundombinu ya Tanesco hususan nyaya zilizoanguka, au
kufanya shughuli yoyote karibu na miundombinu yab umeme katika kipindi
hiki cha mvua kubwa zinazoendela kunyesha nchini. Kulia ni Mhandisi
Simon Kihiyo, na kushoto ni Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila
Muhaji.
Mhandisi Simon Kihiyo, akitoa ufafanuzi wa kitaalamu kuhusu hatua za kuchukua pindi hitilafu ya umeme inapotokea
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...